YOUR WELCOME By ADMIN JERRY KIHUNDO

Let me take this golden chance to welcome everyone around the World,remember that your opinions are very important to us - tanzaniabeautiful.blogspot.com.

M0UNTAIN KILIMANJARO

Kilimanjaro is one of the world's most accessible high summits, a beacon for visitors from around the world. Most climbers reach the crater rim with little more than a walking stick, proper clothing and determination.

MIKUMI

Mikumi National Park abuts the northern border of Africa's biggest game reserve - the Selous – and is transected by the surfaced road between Dar es Salaam and Iringa. It is thus the most accessible part of a 75,000 square kilometre (47,000 square mile)

LET US JOIN TO STOP THIS

No child should be working. Every child has the right to a good education, the right to play and the right to enjoy its childhood. Child labour means that poverty continues to exist. Eradicating child labour means development and better opportunities for everyone.

WE ALL FRIENDS

Everyone is equal in the eyes of God. However people blacks and whites are treated differently in other contries but TANZANIA love and hospitality is our tradition

Friday, March 3, 2017

Lema nje kwa zamana,stori nzima hii hapa!!!!!

Mahakama Kuu Kanda ya Arusha leo inatarajiwa kutoa uamuzi kuhusu maombi ya dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

Ni asubuhi tena kwa mbali jua limeanza kuchomoka huku Arusha ikiwa ni siku ya kupatiwa haki kwa Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema baada ya kuwekwa kizuizini kwa takribani miezi ninachoamini ni kwamba Mahakama kuu leo itatenda haki kwa Lema

Ulinzi nje eneo la mahakamani umeimarishwa sana.
Wananchi wamezuia kuingia mahakama kwenda kusilikiza kesi ya Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Jonathan Lema.

Waandishi wa habari wawili tukiwa nje ya eneo la mahakamani tumekamatwa na Jeshi la Polisi .tumeshikiliwa kwa muda lisaa baada ya majadiliano wahusika tumeachiwa tumezuia kuingia mahakamani.

Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Jonathan Lema akishuka kwenye gari kuingia mahakamani.

Nje eneo la mahakamani wananchi zaidi 23 wamekamatwa na Jeshi la Polisi muda huu wakiwa nje la mahakamani baada ya kuzuiwa kuingia mahakamani kusilikiza kesi ya Mbunge Godbless Jonathan Lema.

Kutoka mahakamani
Wakili wa Serikali ameomba dakika 15 kuwasilisha hoja na Wakili Msomi Peter Kibatala amekubali na kuomba wapewe saa 1 kujibu so Mahakama imehairishwa mpaka saa 7 mchana

Kutoka mahakamani "Virungu vinatembea mahakamani muda huu,watu wanapigwa ,wengine wamekamatwa wamepelekwa central.
Magari ya kuwasha,police wapo na silaha nzito.

Watu wamezuiliwa kuingia,maeneo ya nje ya mahakama ni virungu".

tmp_23435-FB_IMG_14885247387692090696793.jpg 
Viongozi mbalimbali wa Chadema wakiongozwa Katibu Mkuu wa Chadema Dr Vicent Mashinji, Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema Edward Lowasa, Waziri Mkuu Msaatafu Sumaye na Meya wa Jiji la Arusha Mjini Kalisti Lazaro wakiwa mahakamani .
tmp_23435-FB_IMG_1488525644504-1345217214.jpg
Mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe Naibu Katibu Mkuu Chadema John Mnyika ,pamoja na Viongozi mbalimbali wakiwa mahakamani leo.
View attachment 476314 
tmp_7995-FB_IMG_14885273469431093721955.jpg

Viongozi Wakuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wakiwa nje ya Mahakama Kuu ya Arusha baada ya Mawakili wa Jamuhuri kuomba kuwasilisha hoja ambayo wamekwenda kuiandaa kwa dakika 15 na Jopo la Mawakili wa Utetezi likiwakilishwa na Wakili Msomi Peter Kibatala,wameomba dakika 60 ili kujiandaa kujibu hoja hiyo ya mawakili wa Jamuhuri..
tmp_13412-FB_IMG_1488537019231711232815.jpg
Mahakama Kuu Arusha inatarajia kutoa maamuzi ya dhamana na Godbless Lema saa saba na nusu mchana. Mawakili wamepewa muda kujibu hoja zilizotolewa.

Viongozi mbalimbali wa Chadema wanaanza kuingia mahakamani kusubiri uamuzi wa Jaji Magimbi kuhusu dhamana ya Mbunge Godbless Jonathan Lema.

Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Mjini baada ya kupitia hoja za mawakili pande zote imemwachia kwa dhamana Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Jonathan Lema. Ameachiwa kwa dhamana ya masharti ya wadhamini wawili na kusaini bondi ya shilingi milioni moja.