YOUR WELCOME By ADMIN JERRY KIHUNDO

Let me take this golden chance to welcome everyone around the World,remember that your opinions are very important to us - tanzaniabeautiful.blogspot.com.

M0UNTAIN KILIMANJARO

Kilimanjaro is one of the world's most accessible high summits, a beacon for visitors from around the world. Most climbers reach the crater rim with little more than a walking stick, proper clothing and determination.

MIKUMI

Mikumi National Park abuts the northern border of Africa's biggest game reserve - the Selous – and is transected by the surfaced road between Dar es Salaam and Iringa. It is thus the most accessible part of a 75,000 square kilometre (47,000 square mile)

LET US JOIN TO STOP THIS

No child should be working. Every child has the right to a good education, the right to play and the right to enjoy its childhood. Child labour means that poverty continues to exist. Eradicating child labour means development and better opportunities for everyone.

WE ALL FRIENDS

Everyone is equal in the eyes of God. However people blacks and whites are treated differently in other contries but TANZANIA love and hospitality is our tradition

Wednesday, February 7, 2018

Aliye Muua Bob Marley huyu hapa!!!!!

Jasusi wa shirika la kijasusi la Marekeni, Bill Oxley, ndiye binadamu pekee hadi sasa aliyekiri kuhusika moja kwa moja na kifo cha marehemu Bob Marley.

Akiwa katika kitanda cha hospitali ya Mercy huko Miami, Bill Oxley alitoa siri ya muda mrefu kuwa yeye ndiye aliyempa Bob Marley viatu aina ya raba ambavyo ndani yake viliwekwa sindano ndogo sana yenye ncha kali iliyokuwa na vimelea vya ugonjwa wa kansa.

Katika maelezo yake, Bill Oxley anasema alifanya hivyo ikiwa ni mpango wa Marekani kuwaua wanamapinduzi na wapigania uhuru duniani.

"Nilipewa jukumu hilo na kufanikiwa kuwa na urafiki na Bob Marley. Hii ilimfanya asiwe na shaka nilipompa zawadi hiyo ambayo ndoyo iliyoomua," anasema Bill Oxley.

Katika maelezo yake Bill Oxley anaendelea kusema Bado anakumbuka na kuumia sana akijiwa na kumbukumbu ya namna Bob Marley alivyovaa raba hizo kwa furaha na kuhisi kama amechomwa na kitu. Hata hivyo hakuhisi chochote kwani alidhani ni raba zilikuwa zinambana kutokana na kuwa mpya.

Hivyo ndivyo marehemu Bob Marley  alivyoambukizwa kansa iliyoanza kumdhoofisha taratibu hadi alipofariki tarehe 11 Mei 1981 akiwa anatibiwa katika hospitali ya chuo kikuu cha Miami.

Makosa yanayo fanywa kwenye Fedha

💰MONEY MISTAKE 1
Usikope pesa ya riba ili uanzishe biashara. Usitegemee pesa ya mkopo kuianzishia biashara, upate faida kisha uirudishe pesa ya mkopo na riba yake. 

💰MONEY MISTAKE 2
Usitumie pesa ambayo bado haipo mikononi mwako. Wala usije ukamuahidi mtu kumpa pesa ambayo  umeahidiwa mahali fulani. Kama kuna mtu kakwambia, Flan njoo kesho nikulipe deni lako" Basi wewe usiende kukopa vitu kadhaa dukani au hata kumuahidi mtu mwingine kumpa pesa ambayo na wewe umeahidiwa.  Ni kosa. Unaweza kuingia kwenye matatizo.

💰MONEY MISTAKES 3
Kama unataka kuhifadhi/kutunza pesa, kila unapopata pesa usianze kuitumia kwanza kisha ukategemea kutunza kiasi kitakachosalia. Hivyo basi,  ukipata tu pesa,  weka pembeni kiasi unachodhani kinafaa kutunzwa/kuhifadhiwa kisha tumia kiasi kilichobaki. 

💰MONEY MISTAKE 4
Ukipata nafasi ya kuonana na mtu tajiri, kamwe usiombe pesa.  Omba maarifa ya kutengeneza pesa kama yeye, tena kwa mtaji mdogo.  Maarifa ndio mtaji wa kwanza. Unaweza kupewa/kusaidiwa pesa iwapo una mawazo mazuri ya kuzalisha pesa. Baadhi husema,  "Omba ndoano, usiombe samaki"

💰MONEY MISTAKE 5
Usitunze mbegu badala ya kuipanda. Watu wengi hufurahia pesa wanayolipwa/kuipata  kisha wanaiweka bank au nyumbani bila kuiwekeza. Wekeza pesa ili uzalishe zaidi. Usiogope kuingia hasara, kila aliefanikiwa alipoteza kwanza kabla hajafanikiwa. Wengi walipoteza muda, pesa, afya na hata matumaini ya kufanikiwa, ila kwa uthubutu wao, mwisho wa siku walifanikiwa.

💰MONEY MISTAKE 6
Kamwe usimkopeshe mtu pesa ambayo unahisi hatorudisha.  Unapomkopesha mtu huyo pesa,  jiridhishe mwenyewe moyoni kuwa kama hatoweza kulipa basi deni lake halitoathiri urafiki wenu. Ukihisi kwamba kushindwa kwake kulipa kunaweza kuathiri urafiki wenu, basi mshauri aende bank akakope.

💰 MONEY MISTAKE 7
Usikubali uwe shahidi, tena kwa kusaini kabisa ili umdhamini mtu ambae huna uhakika kuwa atalipa kile unachomdhamini. Kumbuka kuwa, dhamana maana yake utawajibika iwapo atashindwa kulipa.

💰 MONEY MISTAKE 8
Epuka kutembea na pesa nyingi ambazo hata huna matumizi nazo wakati huo. Unaweza kujikuta unafanya matumizi ambayo hayakuwa kwenye ratiba sababu ya ushawishi wa pesa ya mfukoni. Ili kuepuka haya, tembea na pesa uliyopanga kuitumia katika safari yako. Pesa nyingine itunze mahali pengine palipo salama. 

💰 MONEY MISTAKE 9
Epuka kutunza pesa mahali pasipo sahihi.  Maeneo kama kwenye soksi, sidiria, chini ya mto wa kulalia, chini ya begi, kwenye kopo au hata kwenye begi la safari, si maeneo salama. Ni rahisi kusahau,  kuibiwa au kupoteza pesa zako. Ni bora ukatunza pesa kieletroniki; yaani bank au kwenye simu au kwenye pochi yenye kamba ngumu ya kuivaa mabegani au wallet ambayo inatosha kwenye mifuko imara na yenye vifungo kwenye nguo zako hasa uwapo safarini. 

💰 MONEY MISTAKE 10
Usitumie pesa kwa kitu ambacho hakikuwa kwenye ratiba yako. Jiulize kwanza kabla hujanunua, "Bila kitu hiki, maisha yataenda au lah? Ukiona maisha yataenda bila kitu hicho, acha kukinunua. Tabasamu kisha ondoka.

💰MONEY MISTAKE 11
Usiingiwe tamaa kwa kununua kitu ambacho ungeweza kununua kwa bei ya punguzo mahali pengine zaidi. Labda tu uwe una pesa nyingi.

💰MONEY MISTAKE 12
Matumizi yako ya pesa yasizidi pato lako. Unaweza kuwa una ndoto kubwa/matumizi makubwa ya pesa kuzidi pato lako.  Unapaswa kuwa bahili katika matumizi yako. Cheza na pato lako. Fanya matumizi makubwa pale tu pato lako litakapoongezeka. Hii itakuepushia kushindwa kufanya baadhi ya mambo ya msingi na kisha ukajikuta unaishia kwenye madeni makubwa. 

💰MONEY MISTAKE 13
Una ndoto kubwa hapo baadae; labda kujenga nyumba, kununua gari, kununua kiwanja, simu nzuri hata pikipiki. Usikurupuke,  ukanunua kitu cha ndoto yako sasa eti tu sababu umekipata kwa bei ya punguzo. Usichanganye kati ya mahitaji ya baadae na ya sasa. Pesa unayotumia kutimizia ndoto sasa itumie kwa mahitaji ya sasa. Ndoto ibaki kuwa ndoto. Hii itakuepushia kuingia katika madeni au kuishi kwa shida sababu ya tamaa. Jipange taratibu kutimiza ndoto yako.

Bila shaka umewahi kufanya moja ya makosa haya. Usirudie kosa. Washirikishe wenzio ili tunufaike sote.

Monday, February 5, 2018

EPL Leo ⚽


Chelsea wapoteza mchezo wa pili mfululizo EPL.
Chelsea 0-3 Bournemouth ..31.01.2018
Watford 4-1 Chelsea.. 5.02.2018

Thursday, February 1, 2018

Kingunge Ngombale-Mwiru Afariki dunia Alfajiri ya leo. >>>>

TANZIA: Mwanasiasa mkongwe, Mzee Kingunge Ngombale-Mwiru amefariki dunia alfajiri ya leo...

Kingunge Ngombale Mwiru ni Mkongwe wa Tanzania na jina lake ni kubwa. Ni mstaafu ambaye katika maisha yake toka ujana wake amelitumikia Taifa mpaka hata ngazi za juu kabisa kama vile kuwa Mkuu wa Mkoa, Mbunge na hata Waziri.

Ni mmojawapo wa vijana wa TANU enzi zao hizo, walioshiriki harakati za kuutafuta uhuru mpaka ukapatikana. Yeye kingunge ndiye aliyekabidhiwa jukumu la kuzigawa kadi mia za kwanza kabisa za wana TANU baada ya TANU kuanzishwa ambapo, Bwana Sykes ndiye aliyezichapisha kwa pesa za kutoka mfukoni mwake.

Kingunge alifanya harakati akiwa karibu na Mwalimu Nyerere, na waliendelea kuwa karibu hata baada ya uhuru kwa majukumu ya kujenga Taifa changa. Kingunge alikuwa ni mmoja wa watu waliokuwa na nafasi nyeti katika TANU na CCM mpaka pale alipoamua kuondoka CCM wakati wa uchaguzi wa mwaka 2015 na kwenda upande wa upinzani.

Source :JamiiForum