YOUR WELCOME By ADMIN JERRY KIHUNDO

Let me take this golden chance to welcome everyone around the World,remember that your opinions are very important to us - tanzaniabeautiful.blogspot.com.

M0UNTAIN KILIMANJARO

Kilimanjaro is one of the world's most accessible high summits, a beacon for visitors from around the world. Most climbers reach the crater rim with little more than a walking stick, proper clothing and determination.

MIKUMI

Mikumi National Park abuts the northern border of Africa's biggest game reserve - the Selous – and is transected by the surfaced road between Dar es Salaam and Iringa. It is thus the most accessible part of a 75,000 square kilometre (47,000 square mile)

LET US JOIN TO STOP THIS

No child should be working. Every child has the right to a good education, the right to play and the right to enjoy its childhood. Child labour means that poverty continues to exist. Eradicating child labour means development and better opportunities for everyone.

WE ALL FRIENDS

Everyone is equal in the eyes of God. However people blacks and whites are treated differently in other contries but TANZANIA love and hospitality is our tradition

Sunday, April 30, 2017

tetemeko Bukoba wananchi wanena

Habari ya muda huu na usiku huu mnene,

Bukoba tena. Tetemeko lililodumu kwa takribani dakika moja na nusu limepita muda huu mjini Bukoba. Baadhi ya wananchi ambao bado tunakumbuka ya tarehe 10/09/2016 tumejikuta tukikimbia nje na watoto wetu.

Sasa nimeanza kuamini Bukoba sio salama sana kwa matetemeko.

Friday, April 14, 2017

Familia ya dinosaria 'Dinasour' yapatikana Tanzania

la-1491957876-g720q3c4l5-snap-image.jpg ​

Mojawapo ya jamii wa awali wa dinosaria alikuwa na maumbile yanayofananishwa na mamba, matokeo ya utafiti Tanzania yanaonyesha.

Wataalam wa masuala ya uhifadhi wa mabaki ya wanyama wamekuwa wakijiuliza familia ya dinosari wa kitambo walifanana vipi, kwani maelezo ya rekodi kutoka enzi hizo ni nadra.

Wengine walidhania walitembea kwa miguu miwili, wakifanana kama dinosari wadogo.

Lakini mnyama mpya aliyeelezewa alitembea kwa miguu minne kama mamba, nakala ya Nature iliripoti

Mnyama huyo mla nyama mwenye urefu wa kati ya mita 2-3 aliyevumbuliwa Tanzania kusini, aliishi takriban miaka milioni 245 iliyopita wakati wa kipindi cha kwanza cha maisha yao (Triassic)

======

Scientists have identified one of the earliest known dinosaur relatives — and it doesn’t look anything like they expected.

Researchers had thought that the oldest dinosaur cousins would look rather like small, two-legged dinosaurs themselves. Instead, Teleocrater rhadinus actually stretched seven to 10 feet long, boasted a long neck and tail, and walked on all fours.

The findings, described in the journal Nature, could force paleontologists to redraw their understanding of dinosaurs’ origins, as well as the nature of the reptiles that came before them.

“This just goes to show that there’s a lot more out there that we just didn’t know, especially the early history of the larger group that dinosaurs belonged to: Archosauria,” said lead author Sterling Nesbitt, a vertebrate paleontologist at Virginia Tech in Blacksburg.

Dinosaurs are part of a larger group known as the archosaurs — a lineage of reptiles that split into a “bird-line” branch that includes pterosaurs, dinosaurs and birds, and a “crocodilian” branch whose living members today include crocodiles and alligators.

Paleontologists have long tried to predict what those early bird-line reptiles looked like, soon after the split with the crocodilian branch. But they haven’t been able to do so because of the large gaps in the fossil record of the transitional period before dinosaurs emerged in the mid-to-late Triassic Period, roughly 230 million years ago. Which dinosaur traits are unique to dinosaurs, and which are shared with these earlier archosaurs, they have wondered? Without a wide range of older archosaur fossils, it was difficult to say for sure.

Still, many figured that the line of animals that gave rise to the flying reptiles known as pterosaurs, and later the dinosaurs, which themselves gave rise to birds (the only surviving member of the bird-line branch) might have originally come from a chicken-sized, two-legged, dinosaur-like archosaur.

The Teleocrater fossils described by Nesbitt and his colleagues may be proving that idea wrong. This species isn’t exactly new to science: Paleontologist F. Rex Parrington first found fossils in Tanzania in 1933 and English paleontologist Alan J. Charig (a posthumous co-author of this paper) characterized the bones roughly two decades later. But the first specimen was missing crucial bones that would have allowed Charig to tell whether this was a bird-branch or crocodile-branch species of archosaur.

la-1491957994-g3o6c21ozo-snap-image.jpg ​

To help fill in those key missing details, Nesbitt and his colleagues studied the original specimen together with three new partial Teleocrater specimens, discovered in 2015 not far from where those original fossils were found. Researchers usually look for certain physical features on the skeleton that remain preserved in a lineage even as species differentiate over time. In the case of Teleocrater, it had a number of markers that identified it as a bird-lineage archosaur, such as a telltale depression on top of the head. It also had a muscle scar high on the thigh bone — a characteristic you see even in chicken legs today. (In crocodilians and in lizards, the muscles are more evenly distributed across the leg.)

But even as Nesbitt and his colleagues identified Teleocrater as a bird-like archosaur, they also found surprisingly crocodilian characteristics, including the animal’s ankle bones. In fact, the entire body plan, with its long, low, four-legged profile, seems in some ways more reminiscent of crocodiles than of theropods, a group of dinosaurs that includes Tyrannosaurus rex and also gave rise to the birds we know today.

“The ankle was really a big surprise with this animal, because all of the archosaurs on the bird side of the tree [including] dinosaurs all have what we call a bird-like ankle, which has a pretty simple hinge, and all the archosaurs on the croc side of the tree have what we call a ‘crocodile normal’ ankle or a crocodile-like ankle,” Nesbitt said. “That tells us that the crocodile ankle was primitive for the earliest archosaurs and that the bird ankle was derived from a crocodile-like ankle.”

This is strange, because that high-thigh muscle scar found in bird-branch archosaurs is typical of animals that walk on two legs — not animals like Teleocrater, which appeared to walk on all fours.

So what explains this weird muscle configuration? For now, it’s unclear, said Nesbitt, who pointed out that many physical features evolved for one purpose before being conscripted into other duties. Feathers, for example, were probably used for insulation, camouflage and even mating displays long before they were repurposed for flight.

“It’s something we see commonly in vertebrate or just animal history,” Nesbitt said.

In any case, that ancient shared ancestor of both crocodiles and dinosaurs (and birds) may have looked more like the former than the latter. And this could change our understanding of which features were originally from early archosaurs, and which emerged much later. It may also cause scientists to reevaluate which ancient archosaurs they study to try to understand what a dinosaur ancestor might have looked like.

The findings, together with other recent discoveries, also highlight how diverse and successful a group the nondinosaur archosaurs were, even if they have fewer representatives among our current fossil records.

“People have concentrated on dinosaurs for a really long time; they were really successful for almost 180 million years and they continue on as successful birds today,” Nesbitt said. “But in the Triassic, they were just a small component of this big radiation of the relatives of dinosaurs.”

Nesbitt and his colleagues plan to return to Tanzania in May to try to fill in more gaps in left in their partial skeletons, and more gaps in our understanding of these long-gone species.

Source: Los Angels Times

Wednesday, April 12, 2017

Historia ya sokoine aliye fariki siku kama ya leo mwaka 1984

*Alimwambia Nyerere apunguze mawaziri akiwemo yeye
sokoine.jpg 
Hii ni gari ya Marehemu Sokoine aliyopata nayo ajali katika eneo la Dakawa Mkoani Morogoro tarehe 12 Aprili 1984 wakati akirejea Dar es Salaam kwa barabara akitokea Dodoma ambako alikuwa akihudhuria Bunge.

SAA 10.00 jioni ile ya Aprili 12, 1984, Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD), sasa Redio ya Taifa ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ilikatiza ghafla matangazo yake ya kawaida, kisha ukapigwa wimbo wa taifa wa “Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania…”


Baada ya wimbo huo kumalizika huku wasikilizaji waliokuwa karibu na redio iwe nyumbani, ofisini na sehemu nyingine wakishangaa na kutaka kujua kwamba kuna nini, wote walipigwa bumbuwazi zaidi waliposikia sauti nzito, sauti ya huzuni na isiyokuwa katika ubora na madoido yake walivyoizoea ikieleza:


“Ndugu wananchi, leo saa saba mchana, ndugu yetu na kijana wetu, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu Edward Moringe Sokoine alipokuwa akisafiri kutoka Dodoma kuja Dar es Salaam, gari yake ilipata ajali. Amefariki dunia!”


Ilikuwa hotuba fupi kuliko zote zilizowahi kutolewa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere tangu akiwa Rais wa Chama cha Tanganyika African National Union (TANU), Waziri Mkuu wa Serikali ya Madaraka ya Ndani (ya Tanganyika), Waziri Mkuu wa Tanganyika huru, Rais wa Tanganyika, Rais wa


Charles Charles

Mwandishi wa makala hii


ni Katibu Msaidizi, Idara ya Itikadi na Uenezi katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam. Anapatikana kwa Simu Na. 0659 220 220 na 0787 088 870


Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na hata vinginevyo.


Ilikuwa ni fupi kuliko zote ikiwa ni ya kwanza na ya mwisho kwake kwa taifa na hata kimataifa, hotuba ambayo hadi leo imebaki ni rekodi katika maisha yake yote akiwa ni kiongozi wa kitaifa na kimataifa.


Hotuba hiyo ilileta jitimai na simanzi kubwa nchini ambapo kwa mfano, akina mama waliokuwa wakiuza maandazi na vitumbua katika eneo la Mtoni Kwa Azizi, Temeke jijini Dar es Salaam ‘walichanganyikiwa’, wengi wakajikuta wakisahau biashara zao na kuanza kukimbia ovyo mitaani huku wakiangua vilio vya kufiwa na mpendwa wao.


Kana kwamba haitoshi, kikao cha Kamati ya Utekelezaji ya Taifa ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kilichokuwa kikifanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, kilisambaratika bila kuahirishwa baada ya Mwenyekiti wake ambaye sasa ni hayati, Sofia Kawawa kuwatangazia wajumbe kuhusu msiba huo mzito na wa ghafla mno.


Kina mama hao wote, kila mmoja utadhani wameamrishwa waliangua kilio kama mtoto aliyekutana na paka mwenye vichwa saba usiku wa manane, kisha wakaondoka na kuachana kama wanyama bila ya kuagana.


Aidha, mwanaume mmoja aliyekuwa akisubiri usafiri wa daladala katika Kituo cha Posta ya Zamani, katikati ya jiji hilo la Dar es Salaam naye alisikika akisema: “Ni bora hata angekufa baba yangu mzazi kuliko kufa kwa Sokoine!”


Edward Moringe Sokoine aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tatu wa nchi hii alizaliwa Agosti Mosi, 1938 huko Monduli Juu, wilaya ya Monduli mkoani Arusha katika familia ya kifugaji.


Aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mara yake ya kwanza Februari 13, 1977 na kutumikia nafasi hiyo hadi Novemba 7, 1980 alipojiuzulu na kwenda kusoma Chuo Kikuu cha Sofia, Bulgaria.


Aliporejea nchini miaka miwili baadaye aliteuliwa tena kushika wadhifa huo Februari 24, 1983 na kuendelea nao hadi alipokufa kwa ajali Aprili 12, 1984 katika eneo la Dakawa (ambalo sasa lipo wilaya ya Mvomero) mkoani Morogoro.


Kifo chake hicho ambacho kilitokea alipokuwa akisafiri kutoka katika kikao cha bunge mjini Dodoma, kilisababishwa na benzi alilokuwa akisafiria kugongwa uso kwa uso na gari aina ya Toyota Land Cruiser iliyokuwa ikiendeshwa na mpigania uhuru wa chama cha African National Congress (ANC) cha Afrika Kusini, Dumisan Dube.


Wakati alipokufa, Sokoine tayari alikuwa amejitengenezea taswira ya uzalendo mkubwa kabisa kwa nchi yake, yule ambaye hadi leo inaaminika kuwa ukimwondoa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, hakuna kiongozi mwingine yeyote wa kisiasa au wa umma aliyefikia uchapakazi wake, uadilifu wake, utendaji wake na hata vinginevyo.


Katika hotuba yake ya mwisho kwa taifa alipokuwa akiahirisha kikao cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma hapo Aprili 11, 1984 alisema:


“Ni kheri mkulima atakayekamatwa akiiba mbolea ili (aende) akaitumie vizuri shambani kwake, huyo (tukidhibitisha hivyo) tutamsamehe, lakini ole wake kiongozi atakayekamatwa kwa (tuhuma za) kufanya ubaridhifu wa mali ya umma”.


Kauli hiyo thabiti katika hali zote ilikuwa ikitoka kinywani mwa mtu na kiongozi aliyekuwa akichukia sana rushwa, ubinafsi na wizi wa fedha za serikali.


Ilitoka mdomoni mwa Waziri Mkuu aliyekuwa akisimamia kauli zake, yule ambaye kile anachosema ndicho alichokuwa nacho moyoni na siyo kwa kuigiza kama wanavyofanya viongozi wengi serikalini, vyama vya siasa na sehemu nyingine za utawala na uongozi wa umma.


Aliishi maisha ya kawaida tofauti na wadhifa wake huo wa juu kabisa ukiwa ni wa tatu baada ya Rais, wakati huo akiwa ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Makamu wa Rais, kipindi ambacho alikuwa Ali Hassan Mwinyi ambaye sasa ni Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Pili.


Alikuwa hajikwezi wala kuishi tofauti na maisha wanayoishi wananchi walio wengi, hivyo ukiondoa tu itifaki za kiserikali alizokuwa ni lazima apewe hakuwahi kabisa kuishi kifahari kama wanavyoishi viongozi wa leo.


Ukiachilia mbali ‘utajiri’ wa ng’ombe alioachiwa urithi na wazazi wake kule Monduli, Sokoine kamwe hakuwahi kumiliki mali nyingine yoyote yakiwemo mavazi ya gharama.


Maisha yake hayo yaliwekwa hadharani na Rais Julius Nyerere wakati wa mazishi ya Waziri Mkuu huyo wa zamani huko Monduli aliposema:


“Edward Sokoine hakuwa na mali yoyote. Ukiacha ng’ombe alioachiwa urithi na wazazi wake alikuwa na mashati matatu, suruali tatu na viatu pea mbili!”


Nani kama yeye?


Bila hata kuwazungumzia mawaziri, naibu mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya ama wabunge kamwe hakuna hata diwani, afisa mtendaji wa kata, mtaa au wa kijiji, mwalimu wa shule ya msingi wala karani tu wa masjala mwenye mashati matatu, suruali tatu na viatu pea mbili tu kama ilivyokuwa kwa Sokoine!


Leo viongozi wetu au watumishi wa serikali wanashindana kwa mavazi, tena ya gharama wakionyeshana nani anayevaa kuliko mwingine.


Wanatambiana kuwa nani anayevaa nadhifu kwa mashati, suruali, suti, viatu, saa au magauni, sketi, blausi na kusuka nywele za gharama kubwa zaidi kushinda wenzake na hata vinginevyo.


Yule anayebadilisha mashati yake matatu, suruali zake tatu, viatu pea mbili, magauni matatu, sketi tatu au blausi tatu huku akisuka nywele za kawaida au kunyoa siku zote anaonekana mshamba na mtu aliyepitwa na wakati!


Maisha yake hayo ya haki ndiyo yaliyompa jeuri ya kukemea aina zote za hujuma, wizi na ubadhirifu wa mali ya umma kama alivyosema katika hotuba yake ile ya mwisho kwa taifa, Dodoma Aprili 11, 1984:


“Ole wao viongozi wanaotumia nafasi za madaraka yao ya umma (kwa ajili ya) kuiba, kuhujumu uchumi au kupokea rushwa maana salama yao ni majaliwa ya Mwenyezi Mungu na labda nisiwajue”.


Mbali na maneno hayo mazito, Waziri Mkuu huyo wa zamani ambaye kifo chake kiliacha kila aina ya simanzi, majonzi na kumbubujisha machozi hadi Mwalimu Julius Nyerere alipouona mwili wake, Ikulu baada ya kufikishwa hapo kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam pia alisema, jana yake kule bungeni:


“Nasikia kuna viongozi wa umma huko mikoani wanagombania magari badala ya kugombania maendeleo ya wananchi, naagiza tabia hii ikome mara moja”.


Hayati Edward Sokoine anakumbukwa pia kwa kusimamia vita dhidi ya wahujumu uchumi kuanzia mwaka 1983 – 1984 alipokufa kwa ajali, ile ambayo hata hivyo “aliondoka nayo kaburini”.


Katika hotuba yake kwa Watanzania wakati wa mazishi ya kiongozi huyo yaliyofanyika nyumbani kwake kule Monduli Juu, Arusha, Baba wa Taifa, wakati huo akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alitoa siri nyingine ambayo ni vigumu kukubalika.


Alisema kwamba kabla ya kifo chake hicho, Sokoine alilalamikia ukubwa wa baraza la mawaziri, hivyo akashauri lipunguzwe na kuwa dogo kulingana na mahitaji na uwezo wa taifa kiuchumi.


Ingawa ushauri huo ungeweza pia kutolewa na mtu mwingine yeyote, kilichomshangaza hata Mwalimu Nyerere ni kauli ya Sokoine kwamba likivunjwa na kuundwa upya, yeye mwenyewe alikuwa radhi na tayari kutoteuliwa tena kama rais huyo wa kwanza wa nchi hii angeona hamhitaji tena!


Sokoine aliyekufa kwa ajali akiwa na umri wa miaka 45, miezi minane na siku 12 kamili alianza elimu yake ya msingi mwaka 1948, kulekule Monduli, wakati huo ikiitwa wilaya ya Masailand alikosoma hadi darasa la nane.


Kutoka huko aliendelea na masomo katika Shule ya Sekondari Umbwe, Moshi mkoani Kilimanjaro alikohitimu darasa la 10 mwaka 1958 na kujiunga rasmi na chama cha TANU mwaka 1961.


Kuanzia mwaka 1962 – 1963 alisomea uongozi na utawala katika iliyokuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Ujerumani Mashariki. Aliporejea nchini, wakati huo akiwa kijana mwenye umri wa miaka 25 aliajiriwa serikalini akiwa Afisa Mtendaji wa Wilaya ya Masailand.


Miaka miwili baadaye aligombea na kuchaguliwa kuwa mbunge wa wilaya hiyo ambayo sasa iliitwa Monduli, fursa iliyompa mwanya wa kuonyesha zaidi kipaji chake kikubwa katika uongozi na utumishi wa umma.


Ilikuwa kipindi hicho ndipo alipoteuliwa kuwa Waziri Mdogo wa Kazi, Mawasiliano na Uchukuzi mwaka 1967, kisha akateuliwa kuwa Waziri wa Nchi Katika Ofisi ya Rais (Usalama) ilipofika mwaka 1970.


Miaka miwili baadaye hapo mwaka 1972, Sokoine aliteuliwa na Rais Julius Nyerere kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa hadi Februari 13, 1977 alipoteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kubadilishana nafasi na mtangulizi wake, Rashid Mfaume Kawawa.


Akiwa amechaguliwa kwa mara yake ya tatu mfululizo kuwa Mbunge wa Monduli mwaka 1975, Sokoine aliingia kwa mara ya kwanza pia katika ujumbe wa Kamati Kuu ya TANU, kisha akawa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM mpaka Novemba 7, 1980 alipojiuzulu nafasi ya Waziri Mkuu kwa matakwa yake mwenyewe.


Alirejea katika chombo hicho cha juu kabisa kisiasa alipoteuliwa tena kuwa Waziri Mkuu wa nchi hii ilipofika Februari 24, 1983 hadi Aprili 12, 1984 alipopata ajali ile barabarani, eneo la Dakawa, Morogoro na kufa papo hapo.


Katika kutambua mchango wake mkubwa kwa taifa, serikali ilikigeuza kilichokuwa Kitivo cha Kilimo cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kampasi ya Morogoro na kuwa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, maarufu kwa kifupi cha SUA.


Historia inaonyesha kwamba kilianzishwa mwaka 1964 kama Chuo cha Kilimo kilichokuwa kinafundisha na kutoa stashahada (au diploma) za kilimo, kisha kikapandishwa hadhi na kuwa Kitivo cha Kilimo cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hapo mwaka 1969.

Akiwa ni kiongozi mwandamizi wa taifa, Sokoine anakumbukwa hadi leo, miaka 32 baada ya kifo chake siyo kwa sababu alikuwa Waziri Mkuu kwani wadhifa huo umeshashikwa pia na wanasiasa wengine akiwemo mrithi wake alipofuka mwaka 1984, Balozi Dk. Salim Ahmed Salim.


Wengine waliowahi kushika wadhifa huo ukimwondoa Mwalimu Julius Nyerere, Kawawa na Waziri Mkuu wa sasa, Majaliwa Kassim Majaliwa ni Cleopa David Msuya, Joseph Sinde Warioba, John Samwel Malecela, Frederick Tluway Sumaye, Edward Ngoyai Lowassa pamoja na Mizengo Kayanza Pinda.


Hayati Sokoine anakumbukwa hadi leo kwa sababu aliamini, kusimama na kupigana kwa vitendo ili kutetea haki kwa wote, usawa usiokuwa na ubaguzi pamoja na uwajibikaji kazini katika utumishi wa umma.


Alikuwa ni mzalendo wa kweli aliyeishi na kuamini katika misingi halisi ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, kiongozi ambaye wakati wake wote alikuwa mchapakazi na mtu asiyejua kujikweza.


Ndiyo maana alifanya kazi mpaka usiku wa manane na hata alipokuwa barabarani akipitia mafaili na nyaraka mbalimbali, akatoa maelekezo ya kufanya kwa wasaidizi wake kuanzia ofisini hadi mawaziri, wakuu wa mikoa na watendaji wengine serikalini.

Alikuwa akichukia na kupambana kwa nguvu zake zote dhidi ya vitendo vyote vinavyohusu ubadhirifu wa fedha na mali za umma, wizi wa aina zote, kutowajibika au uzembe kazini hususan katika utumishi wa umma, rushwa, uhujumu uchumi, ulanguzi pamoja na magendo.


Aliamini kuwa “Siasa ni Kilimo” na ndiyo maana siku zote aliipigania sekta hiyo kwa kauli na vitendo. Alitaka Tanzania ijitosheleze yenyewe kwa chakula, iiuze nje ya nchi ziada na kuzalisha kwa wingi mazao yote ya biashara kama ya pamba, kahawa, chai, mkonge, kakao na kadhalika ili kuliingizia taifa fedha za kigeni.


Alifanya hivyo akiamini pia kuwa kilimo ni uti wa mgongo. Hakutaka taifa liwe ombaomba ila lenye nguvu kiuchumi. Ndiyo maana alijitahidi kuliwekea msingi imara wa maendeleo kupitia elimu ya kujitegemea na siyo ya kutafutia kuajiriwa.


Ndiyo maana hadi leo, Jumanne Aprili 12, 2016 ikiwa ni miaka 32 kamili baada ya kifo chake kilichotokea kwa ajali ya barabarani Aprili 12, 1984, Watanzania bado wanazidi kumlilia utadhani amekufa jana na kushindikana kabisa kumsahau.


Mungu aendelee kuiweka roho yake mahali pema peponi. AMEN!

Mwandishi wa makala hii Charles Charles ni Katibu Msaidizi, Idara ya Itikadi na Uenezi katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam. Anapatikana kwa Simu Na. 0659 220 220 na 0787 088 870
sokoine2.jpg 

Katika nchi inayojali haki na usawa, Majeshi hayana budi yawe ni chombo cha kulinda haki na maslahi ya walio wengi. Na kamwe hayaruhusiwi kuwa ni chombo cha wachache wenye kujali nafsi zao na kusahau maslahi ya walio wengi" - Edward Moringe Sokoine, 1Februari 1977

Saturday, April 8, 2017

Roma amepatikana

Msanii Roma Mkatoliki anadaiwa kupatikana na yupo Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar.

Habari ya akina Roma kupatikana imethibitishwa na Mkurugenzi wa Tongwe Records J. Mada.

Bado hakuna maelezo ya kutosha kuhusiana na wapi walipokuwa na nani waliokuwa wamewashikilia. Kwa sasa wanadaiwa kuwepo kituoni hapo kwa taratibu za kipolisi kwa kuwa jalada la kupotea kwao lilifunguliwa hapo.

Kupatikana kwao kumefuatia wito mkubwa uliokuwa ukipaishwa na wasanii wenzake na mashabiki kuhusu kuachiliwa huru, ndani na nje ya mitandao ya kijamii.

Awali, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishina Simon Sirro alisema bado walikuwa wakiendelea na upelelezi wa tukio la kupotea (kutekwa) kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake.

Taarifa zaidi zinafuata..

ROMAA.png 
roma.jpg